Sura ya pili [2]

15 Matumizi ya Lugha

SARUFI: KUWA NA

Kitenzi kuwa kinatumika katika tensi mbalimbali zinazoitwa Tensi za Maneno Mawili, kama vile nilikuwa nikisema, ‘I was saying’, n.k. (=na kadhalika). Kitenzi kuwa na, ‘to have’ kinatumika zaidi.

Zoezi la kwanza. WAKATI ULIOPITA; WAKATI ULIOPO.
Badilisha sentensi kama unavyoonyeshwa katika mfano.
*            Regina alikuwa na watoto watano.
–>         A: Kumbe, Regina ana watoto watano?
B: Ndiyo, anao.
_______________________________________
1          Chumba kilikuwa na watoto.
2          Wachawi walikuwa na nguvu.
3          Namagondo ilikuwa na nyumba chache.
4          Samaki alikuwa na miba.
5          Mzigo ulikuwa na kufuli.
6          Honorata alikuwa na shamba la pamba.
[Pattern translated: * Regina had five children. –> A: So Regina has five children? B: Yes, she does (have them).]


Zoezi la pili. KANUSHA WAKATI ULIOPITA.
Badilisha sentensi katika Zoezi la pili kama unavyoonyeshwa katika mfano.
*             Regina alikuwa na watoto watano.
–>          A: Kumbe nimesikia eti hakuwa na watano.
B: Kumbe!
_________________________________________
[Pattern translated: * Regina had five children. –> A: Hm, I heard that she didn’t have five. B: Hm!]


Zoezi la tatu. KANUSHA WAKATI UJAO.
Tunga sentensi zenye sarufi hii ukitumia picha za kutoka mtandaoni, kama AfricaFocus: http://africafocus.library.wisc.edu/
atakuwa na (s/he will have)
hatakuwa na (s/he won’t have)

License

Icon for the Creative Commons Attribution-NonCommercial-ShareAlike 4.0 International License

Mazoezi ya Rosa Mistika Copyright © by Magdalena Hauner is licensed under a Creative Commons Attribution-NonCommercial-ShareAlike 4.0 International License, except where otherwise noted.

Share This Book

Feedback/Errata

Comments are closed.